Fri, 17 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limekataa maombi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuruhusu Mashabiki kwenye mechi kati ya Biashara United na FC Dikhil ya Djibouti.
Mechi hiyo ya marudiano ya Kombe la Shirikisho la CAF itachezwa Jumamosi, Septemba 18 mwaka huu saa 1 kamili jioni Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
CAF imesisitiza kuwa mechi zake zote zitachezwa bila Mashabiki kama ilivyoainishwa katika mwongozo wake na ule wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kuhusu ugonjwa wa Covid-19.
Sehemu ya taarifa ya TFF
Chanzo: www.tanzaniaweb.live