Tue, 6 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkataba wa Karim Benzema katika timu ya Al Ittihad, utamfanya apokee Euro milioni 200, ambazo ni zaidi ya Sh bilioni 500 za Tanzania kwa mwaka.
Mkataba wa Benzema utaisha Juni 2025 ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja, kwa mujibu wa mwandishi wa habari za michezo, Fabrizio Romano.
Romano amesema mkabata umeshasainiwa na muda wowote kuanzia sasa klabu hiyo itatoa taarifa rasmi. Mfaransa huyo anatarajiwa kutambulishwa mara baada ya taarifa ya Al Ittihad.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live