Kama kuna kitu fundi Karim Benzema anakipenda baada ya soka, basi ni magari makali.
Mshambuliaji huyo maarufu wa Real Madrid amekuwa akiyaonyesha baadhi ya magari hayo ya kifahari kupitia mtandao wa Instagram.
Benzema (35) anamiliki Bugatti Veyron lenye thamani ya takribani pauni milioni 1.5, mwaka 2021 aliongeza Bugatti Chiron lenye thamani ya takribani pauni milioni 2.5 vilevile ana Ferrari 458 Spider na mengine mengi.
Pembeni ya magari ya kununua, wataalamu wajanja wa masoko husababisha watu kama Benzema kuweza kuwa na magari ya kifahari mara kwa mara.
Mfano, kampuni ya kijerumani ya Audi ambayo hudhamini klabu ya Real Madrid huwapatia wachezaji hao karibia kila mwaka magari ya kisasa kama sehemu ya kujitangaza.