Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benzema Shujaa mpya Real Madrid

Karim Benzema With Marcelo Benzema akiwa na Marcelo

Sun, 1 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Karim Mostafa Benzema ndio jina la halisi la shujaa mpya wa Real Madrid aliyeiongoza timu hiyo kutwaa ubingwa wa 35 wa ligi kuu ya Hispania La Liga na kuweka kumbukumbu isiyo sahaulika kwenye msimu 2021-22.

Karim Benzema siku ya jana alifunga goli lake la 26 kwenye michezo 30ya ligi huku akiwa moja ya watu waliohakikisha Espanyol wanaondoka Bernabeu kwa kipigo cha 4-0 na kuhakikisha madrid anatawazwa kuwa bingwa wa La liga.

Karim Benzema alisajiriwa na Real madrid mwaka 2009 akitokea ufaransa kwenye klabu ya Lyon huku akiwa mchezaji kutoka ufaransa aliyenunuliwa kwa pesa kubwa kwa mwaka huo, ambapo Madrid walilipa €35 million. na tokea ajiunga na klabu hiyo amefanikiwa kuwa kuchaguliwa kwenye kikosi bora cha la liga 2018/19, 2019/20 na 2020/21

Pia amekuwa mfungaji bora wa timu hiyo akishika nafasi ya tatu na mtoa basi bora za magoli wa muda wote na amekuwa mchezaji bora wa ligi kwenye msimu 2019-20. wakati akiwa mchezaji wa real madrid alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa ufaransa mara nne.

Benzema kwenye miaka yake 11 aliyoitumika klabu ya Real Madrid amefanikiwa kuchukua makombe 21 yakiwemo, La liga , Copas del Rey na klabu bingwa barani Ulaya,

Baada kuondoka kwa Ronaldo, benzema amekuwa ndio kiongozi wa safu ya ushambuliaji na mfungaji tegemezi, huku akifunga magoli 30 na kutoa pasi za mwisho 11 kwenye msimu wa 2018/19, msimu wa 2019/20 magoli 27 pasi za mwisho 11 na msimu wa 2021/22 mpaka sasa ana mgoli 42 kwenye michezo 42.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live