Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Beno awatumia salam Simba "Soka sio vita"

Ry Benooo Beno awatumia salam Simba "Soka sio vita"

Thu, 3 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Golikipa wa Singida Fountain Gate FC, Beno Kakolanya amewatumia salam waajiri wake wa zamani, Simba SC kuwa kikosi chake kinajifua vilivyo kuelekea mchezao wao wa Ngao ya Jamii utakaopigwa katika Dimba la Mkwakwani Tanga, Alhamisi ijayo, Agosti 10 2023.

Beno ambaye alikuwa Simba kabla ya kujiunga na Singida amesema kuwa amepata mapokezi makubwa ndani ya SIngida BF hivyo ana deni kubwa la kuhakikisha anafanya vyema kuisaidia timu yake hiyo mpya.

Singida FG jana ilicheza mchezo wake wa kirafiki na AS Vita Club ya Vongo na kuibuka na ushindi wa bao 2-1 katika Tamasha la Singida Big Day maalum kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wao wapya.

“Mpakja mashabiki wananishangilia vile inaonyesha wana Imani kubwa na mimi na kuna kitu wanakitarajia kutoka kwangu, nimefurahi kwa mapokezi walionipa.

“Kuelekea mechi dhidi ya Simba, niwaombe mashabiki wa Singida wawe na Imani na timu yao, kwa sasa tunaendelea kujifua ili kutengeneza muunganiko kwa sababu wachezaji wengi ni wapya, kwa hiyo mpaka mechi ya Simba itakapofika tutakuwa tumekaa vizuri, mpira sio vita.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live