Wed, 6 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Benin, imewasili usiku wa Oktoba 5 katika Uwanja wa Julius Nyerere International Airport Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Afisa Habari wa TFF, Clifford Mario Ndimbo, amethibitisha kuwasili kwa kikosi hicho.
"Ni kweli timu ya Benin imeshawasili ikiwa na msafara wa watu 70, na wanatarajia kufanya mazoezi siku ya leo katika uwanja wa mkapa majira ya sa kumi jioni" amesema Ndimbo
Benin itakabiliana na Tanzania Oktoba 7, katika Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za kombe la dunia Qatar 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live