Fri, 16 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kipa wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England, Ben Foster (39) ametangaza kustaafu soka.
Foster alimaliza mkataba wake na klabu ya Watford mwishoni mwa msimu uliopita na alikataa ofa ya kujiunga na klabu ya Newcastle kwa msimu huu.
Kipa huyo alithibitisha kustaafu kwake kupitia video iliyowekwa kwenye channel yake maarufu katika mtandao wa Youtube, video hiyo iliambatana na ujumbe uliosema "ni wakati wa kusema kwaheri."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live