Sat, 8 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliekuwa Beki wa kushoto wa Ihefu Yahaya Mbegu ametambulishwa katika Klabu ya Singida Fountain Gate leo Julai 8, 2023.
Kupitia kurasa zake za mitandao ya Kijamii Singida FG wameandika;
"Katika kuimarisha safu yetu ya ulinzi, tumemuongeza beki mpya wa kushoto ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chetu kwa mkataba wa miaka mitatu."
Karibu sana BIG STAR Mbegu!
Mbegu alikuwa anatajwa kumalizana na Simba waliokuwa wanamtazama kuziba pengo la Gadiel Michael aliepewa Thank You siku chache zilizopita.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live