Inaelezwa kuwa beki wa kati wa kimataifa wa Yanga kutoka Mali, Mamadou Doumbia wakati wowote atapewa ‘Thank You’.Habari zinaeleza kuwa tayari Yanga imeshamalizana na beki huyo ikiwa na malengo ya kuingia sokoni kusaka mbadala wake.
Beki huyo alisajiliwa Yanga dirisha dogo kwa mkataba wa miaka miwili akiwa mchezaji huru na sasa Yanga watalazimika kuvunja mkataba na watamlipa kiasi cha dola 50,000 (Sh 120milion)
Kwa msimu wa 2022/23 beki huyo hajawa chaguo la kwanza chini ya Nasreddine Nabi licha ya kuwa alikuwa ni ingizo jipya kwenye dirisha dogo.
Tayari Yanga imeachana na baadhi ya nyota wake ikiwa ni pamoja na Dickson Ambundo, Bernard Morrison, Tuisila Kisinda na Eric Johora.