Klabu ya Al Nassr Fc ya Saudi Arabia imethibitisha kusitisha mkataba na beki zamani wa Manchester United Alex Telles kwa makubaliano ya pande zote mbili na sasa nyota huyo wa zamani wa FC Porto ni mchezaji huru.
Klabu ya Al Nassr Fc ya Saudi Arabia imethibitisha kusitisha mkataba na beki zamani wa Manchester United Alex Telles kwa makubaliano ya pande zote mbili na sasa nyota huyo wa zamani wa FC Porto ni mchezaji huru. Telles (31) raia wa Brazil alijiunga na klabu hiyo mwaka jana 2023 kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Manchester United ambapo ameichezea Al Nassr Fc mechi 44 ikiwemo michezo minne msimu huu.