Thu, 11 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mke wa mchezaji wa ‘klabu’ ya Manchester City Kyle Walker, Annie Kilner ametangaza kutengana na mume baada ya kudumu kwa miaka miwili kwenye ndoa.
Kwa mujibu wa The Sun News imeeleza kuwa mwanadada huyo ameamua kuachana na ‘beki’ huyo wa kulia, baada ya kugundua kuwa #Walker anamsaliti na wanawake wengine.
Wawili hao ambao walikuwa katika mahusiano kwa zaidi ya miaka 12 walifunga ndoa Disemba 2021 na kubahatika kupata watoto watatu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live