Gwiji wa zamani wa soka na mmiliki mwenza wa klabu ya soka ya Marekani ya Inter Miami, David Beckham, amemuajiri mlinzi wa kumlinda mshambuliaji wa timu hiyo, Lionel Messi dhidi ya usumbufu ambao unaweza kutokea nje ya uwanja.
Mlinzi huyo ajulikanae kwa jina la Yassine Cheuko, ni mwanajeshi mstaafu wa jeshi la Marekani aliepigana vita vya Iraq na Afghanistan kabla ya kustaafu na kuamua kuwa mkufunzi na mchezaji wa ngumi za MMA na Taekwondo.
Mlinzi huyo amekuwa akionekana kwenye mitandao ya kijamii akiwa na na mkali huyo wa Argentina kila mahali kuhakikisha usalama wake.
Tazama Video hapa Chini;
Cheki umakini wa mlinzi wa Messipic.twitter.com/RwlIqEL9SQ
— MASSAY, Elifuraha Joshua (@Elifuraha_JM) August 24, 2023