Thu, 15 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Bayern Munich inadaiwa kuwa imeshindwa kumchukua mchezaji wa ‘klabu’ ya Chelsea Mykhailo Mudryk baada ya ‘timu’ hiyo kukataa ofa ya Bayern Munich.
Kwa mujibu wa The Sun News inaelezwa kuwa Munich ilikuwa katika hatua za mwisho za kumnunua mchezaji huyo lakini mwezi uliyopita Chelsea ilikataa ofa hiyo, huku sababu za ombi hilo kukataliwa bado hazijajulikana.
Mchezaji huyo kutoka nchini Ukraine, mwenye umri wa miaka 23, alijiunga na Chelsea Januari 2023, kwa mkataba wa pauni 97 milioni akitokea ‘timu’ ya Shakhtar Donetsk.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live