Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bayern Munich waingilia dili la Kim Minjae

IMG 4334 Kim Minjae.jpeg Kim Minjae

Sun, 18 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mabingwa wa Soka nchini Ujerumani FC Bayern Munich huenda ikaipundua Manchester United kwenye dili la kuiwania huduma ya beki kisiki wa SSC Napoli, Kim Minjae katika dirisha la usajili wa majira ya Kiangazi, kufuatia ya mchezaji huyo kuonyesha uhitaji zaidi wa kutaka kuichezea Munich kuliko Man United.

Fundi huyu wa kimataifa wa Korea Kusini alidaiwa kufikia makubaliano binafsi na Man United lakini sasa mambo yanaonekana kubadilika na huenda akatimkia zake Ujerumani.

Kim ameshawishika zaidi na ofa ya Munich kwa sababu anaona huko ndio ataweza kushinda mataji tofauti na Man United ambapo timu ndio inajengwa kwa sasa.

Staa huyu amezivutia timu nyingi barani Ulaya kutokana na kiwango alichoonyesha msimu huu akiwa na Napoli ambayo ameisaidia kuchukua ubingwa wa Italia.

Inadaiwa ili kuipata huduma yake, Napoli inataka ofa isiyopungua Pauni 40 milioni. Kwa msimu uliopita fundi huyu amecheza mechi 45 za michuano yote. Mkataba wake unamalizika mwaka 2025.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live