Thu, 23 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Atalanta imetwaa ubingwa wa Ligi ya Europa baada ya kukomesha rekodi ya Ulaya ya kutopoteza (unbeaten) 51 iliyokuwa ikishikiliwa na Bayer Leverkusen kufuatia ushindi wa 3-0 dhidi ya Mabingwa hao wa Bundesliga katika dimba la Aviva, Dublin
Mabao ya Atalanta katika mchezo huo uliopigwa jana Mei 22, yamefungwa na Ademola Lookman 12’26’ na 75’.
Matumaini ya Xabi Alonso na vijana wake ya kutwaa makombe matatu (treble) yamefikia ukomo baada ya kukubali kichapo cha kwanza cha msimu huku Mnigeria Ademola Lookman akifunga hat-trick ya kwanza kwenye fainali ya Ligi ya Europa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live