Fri, 5 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo Mshambuliaji wa Inter Milan, Nicolo' Barella, amesaini mkataba utakaomuweka klabuni hapo mpaka Juni 2026.
Barella ambae aliwindwa sana na vilabu vikubwa barani Ulaya katika dirisha la usajili lilopita, anatarajiwa kukunja kiasi cha Euro milioni tano kama mshahara wake.
Barella ameshinda Kombe la Euro mwaka huu akiwa na kikosi cha Italia na ameonyesha kiwango bora ambacho kilisababisha vigogo kadhaa kumuwania.
Barella vile vile anapendekezwa kuwa Nahodha wa Inter Milan msimu ujao wa 2022/2023.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live