Ferran Torres amefunga goli la penati na kuipatia Barcelona alama moja kuelekea mchezo wa marudiano dhidi ya Napoli katika sare ya 1-1 mtanange wa Ligi ya Europa uliopigwa Alhamis dimba la Camp Nou hatua ya 32.
Wakicheza kwa mara ya kwanza michuano hiyo baada ya angalau miaka 18, wababe hao wa soka la Hispania walijikuta wako nyuma kupitia bao la Piotr Zielinski wa Napoli.
Wakati upande wa Barcelona goli lao lilitokea kupitia matumizi ya video saidizi kwa refarii ambapo ilimuonyesha mlinzi Juan Jesus akiunawa mpira wa krosi ya Adama Traore.
Baada ya VAR hatimaye penati ikaamuriwa kupigwa, Torres akakwamisha mpira huo kwa kumpoteza kipa Alex Meret.
Kwa matokeo hayo, Barcelona watahitaji kushinda mchezo wa mkondo wa pili utakaopigwa Italia Februari 24, 2022 ili kufuzu hatua ya 16 bora ya Ligi ya Europa.