Thu, 11 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
FC Barcelona imekanusha taarifa za kuwa ipo mbioni kumrejesha beki wa zamani Mbrazili, Dani Alves katika kikosi hicho ili kuongeza nguvu kutokana na mwanzo mbovu wa timu hiyo msimu huu.
Alves mwenye umri wa miaka 38 yupo huru baada ya kumaliza kandarasi yake na Sao Paulo, amesema yeye yupo tayari kwenda kuongeza nguvu ndani ya kikosi hicho kama watamuhitaji.
Uongozi wa klabu umesema jukumu la usajili wamemuachia kocha wao, Xavi Hernandez lakini Dani Alves siyo sehemu ya mipango yao.
Dani Alves na Xavi Hernandez, waliwahi kukipiga pamoja Barcelona, chini ya kocha Pep Guardiola.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live