Mon, 20 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Barcelona imeendelea kuwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu nchini Hispania La Liga baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Cadiz wakiwa dimba la nyumbani Camp Nou.
Ushindi huo unaifanya Barcelona kuwa kileleni kwa tofauti ya pointi nane dhidi ya Real Madrid waliopo nafasi ya pili.
Mabao ya Barcelona yakiwekwa kambani na Sergi Roberto kabla ya Roberto kutengeneza bao lingine kwa mshambuliaji kinara wa La Liga Robert Lewandowski ambaye sasa anafikisha goli 15 bao nne zaidi ya Karim Benzema.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live