Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Barcelona wavunja mkataba na Ramon Planes

Planes Ramon Planes

Wed, 17 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Barcelona wametangaza rasmi kuvunja mkataba na katibu wao Ramon Planes kwa maombi yake mwenye bwana Ramon Planes ambaye alitaka kuachana na klabu hiyo.

Planes alikuwa na mkataba na klabu hiyo ambao ulikuwa unaisha majira ya kiangazi mwaka 2022, lakini Planes ameamua kuvunja mkatba wake na klabu ya Barcelona ili akatafute changamoto sehemu nyingine.

Planes alifanya kazi kubwa kwenye mikakati ya usajiri katika kipindi chake alichokuwepo kwenye viunga vya Camp Nuo, na alikuwa mtu muhimu kwenye usajiri wa Pedri na Ronald Araujo pia alihakikisha maendeleo ya makinda kama Gavi na Ilaix Moriba.

Ramon Planes aliteuliwa na raisi wa Barcelona aliyepita Josep Maria Bartomeu na alifanya kazi na Eric Abidal na aliendelea na kazi yake hiyo hata baada ya Abidal kuondoka, na alikuwa mtu muhimu sana kwa kocha Ronald Koeman.

Tokea Xavi ametangazwa rasmi kuwa kocha wa timu Barcelona amefanya mabadiliko karibia kila idara inayohusika moja kwa moja na maendeleo ya wachezaji kuanzia madaktari na idara nyingine mbali mbali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live