Klabu ya Barcelona jana imemtambulisha mchezaji wao mpya, Philippe Coutinho kwa ushindi mzito wa magoli 3-0 dhidi ya klabu ya Levante.
Philippe Coutinho
Magoli ya Lionel Messi, Luis Suarez na Paulinho yameifanya klabu hiyo kuongoza kwenye msimamo wa Ligi Kuu soka Hispania (La Liga).
Wakati hayo yakijiri mahasimu wakubwa wa Barcelona, Real Madrid wamepata sare ya goli 2-2 dhidi ya Celta Vigo.
Kwa matokeo hayo Barcelona inaongoza Ligi kwa alama 48 ikifuatiwa na Atletico Madrid wenye alama 39 huku Madrid wakiwa nafasi ya 4 kwa alama 32.
Tazama picha za Coutinho alivyokaribishwa na Barcelona jana kwenye uwanja wa Nou Camp;