Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Barcelona waendelea kukimbiza La Liga

Barca Beat Sevilla Barcelona imeshinda magoli 3-0 dhidi ya Sevilla

Mon, 6 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Barcelona wamefaidika na matokeo ya hivi punde ya Real Madrid ambaye amepoteza jana huku wao wakiifunga Sevilla mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Camp Nou na kusonga mbele kwa pointi nane kileleni.

Real Madrid walipata kipondo cha 1-0 kutoka kwa Real Mallorca mapema jana ambacho kilifungua milango kwa Barca, ambao walipata ushindi wao wa 10 mfululizo msimu huu huku wakiwa vinara.

Barca walilazimika kufanya mabadiliko ndani ya dakika nane za mwanzo baada ya Sergio Busquets kuumia kifundo cha mguu na wakapata tabu sana katika kipindi cha kwanza.

Wakati mabingwa watetezi Madrid wakiendelea kutatizika kupata uthabiti wowote, Barca sasa wameshinda michezo 10 kati ya 11 ya LaLiga na hawajafungwa tangu katikati ya Oktoba.

Ushindi huu wa hivi karibuni wa Xavi walistahili dhidi ya Sevilla ambayo ilikuwa imeshinda mechi mfululizo, huku vijana wa Xavi wakionyesha makali ya kuwa mabingwa katika kipindi cha pili.

Sevilla sasa wameshindwa kuifunga Barca katika mechi 15 za LaLiga na hawajashinda Camp Nou kwenye ligi katika michezo 20 tangu Desemba 2002.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live