Bao pekee la Hakan Calhanoglu dakika ya 45 na ushei limeipa Inter Milán ushindi wa 1-0 dhidi ya Barcelona katika mchezo wa Kundi C usiku wa jana Uwanja wa Giuseppe Meazza Jijini Milan.
Bao pekee la Hakan Calhanoglu dakika ya 45 na ushei limeipa Inter Milán ushindi wa 1-0 dhidi ya Barcelona katika mchezo wa Kundi C usiku wa jana Uwanja wa Giuseppe Meazza Jijini Milan. Kwa matokeo hayo, Inter Milan wanafikisha pointi sita na kusogea nafasi ya pili, wakizidiwa pointi tatu na Bayern Munich, wakati Barcelona inabaki na pointi zake tatu nafasi ya tatu baada ya wote kucheza mechi tatu.