Wachezaji wawili wa kutokea bechi Ferran Torres na Memphis Depay wamefunga mabao na kuipa Barcelona alama tatu muhimu mbele ya timu iliyoonyesha ushindani wa hali ya juu ya Elche mchezo wa Ligi Kuu nchini Hispania La Liga uliomalizika 2-1.
Elche ambao wako nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi hiyo walipata bao la kuongoza kupitia kwa nahodha Fidel aliyetumia makosa ya kiungo Pedri.
Hata hivyo, kipindi cha pili kocha Xavi alifanya mabadiliko ambayo yalitosha kuwapa nguvu hasa kwa Torres ambaye aliongeza kasi ya mchezo na kupelekea goli lake na la ushindi kwa mkwaju wa penati iliyofungwa na Depay.
Ushindi wa Barca unaifanya kupanda mpaka nafasi ya tatu ingawa wanaweza kukaa kwa muda endapo Real Betis watashinda kwa Atletico Madrid.