Wababe wa Catalunya wanapambana kwa kila hali kuhakikisha wanafuzu hatua ya 16 ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, baada ya kuwa michezo yake ya awali haikupata matokeo chini ya Ronald Koeman.
Bao pekee la Ansu Fati limeipa Barcelona ushindi wa 1-0 dakika ya 70 limeipa Barcelona ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Dynamo Kyiv usiku wa Jumanne Uwanja wa NSK Olimpiki.
Barca inafikisha pointi sita na kupanda nafasi ya pili ikizidiwa pointi sita na vinara, Bayern Munich wakati Dynamo Kyiv inabaki na pointi yake moja katika nafasi ya tatu nyuma ya Benfica yenye pointi nne baada ya wote kucheza mechi nne.