Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Barbara azidi kukichafua huko Twitter

Barbara Ya Barbara azidi kukichafua huko Twitter

Fri, 14 Jul 2023 Chanzo: Bbc

Aliyekuwa CEO wa Simba SC, Barbara Gonzalez ameendelea kukinukisha huko Twitter kwa kuandika jumbe zake tata.

Mapema hii leo Julai 14, 2023, Barbara ameweka ujumbe mpya uliosomeka hivi:

"Ulevi wa madaraka haujawahi kuwa na mwisho mwema."

Kama kawaida ujumbe huo umezua mjadala na watu kuhoji ni kitu gani kilichopo nyuma ya jumbe hizo zinazoonekana kama kuna watu anawalenga.

Kabla ya ujumbe huo, Barbara aliandika jumbe nyingine tata ambazo pia ziliibua mjadala wa kutosha.

"Usilipize ubaya kwa ubaya, lakini usiwe mnyonge kudai haki zako!"

"Hauwezi kudhulumu haki za watu halafu ukataka amani na mafanikio."

Chanzo: Bbc