Nyota raia wa Zambia, Barbara Banda ameweka rekodi ya kuwa nambali mbili katika orodha ya wachezaji ghali wa kike ulimwenguni
Kwa Mujibu wa transfer market nahodha huyo wa Zambia amefikia rekodi hiyo baada ya kukamilika Kwa uhamisho wake kutoka Shanghai Shengii ya China kwenda Orlando Pride ya USA Kwa ada ya $ 780,000 ambayo ni sawa na Bilioni 1.9 kwa pesa ya Tanzania
Kinara huyo wa Copper Queens alikuwa ni mchezaji wa kwanza kufunga hat trick katika Olympic ya Tokyo Japan na kumuongezea thamani zaidi mpaka kuhitajika na klabu ya Shanghai
Anayeshika nafasi ya kwanza katika orodha ya wachezaji ghali wanawake ni Mshambuliaji wa Chelsea Mayra Ramirez baada ya kukamilisha usajili wake mwezi Januari kutokea Levante.