Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro amethibitisha kuwa bao la Mama ( Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan) limepanda kiwango kwenye Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF).
Waziri Ndumbaro alisema kiwango cha pesa kimepanda kutoka Sh. Milioni Tano katika hatua ya makundi hadi Sh. Mil 10 katika hatua ya Robo Fainali.
Rais Samia amekuwa na utaratibu wa kutoa pesa kwa timu za Simba SC, Yanga SC Taifa Stars ili kuongeza hamasa katika michezo yake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live