Sat, 26 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa Richardsbay FC au Natal Rich Boys, Mtanzania Abdi Banda ameshinda kesi aliyoifungua dhidi ya timu yake ya zamani Chippa United ambayo sasa inatakiwa kumlipa Randi 4.5 milioni (sawa na Sh 600 milioni).
Kupitia mwanasheria wake, Lyrique de Plessis raia wa Uingereza, Banda alifungua kesi FIFA kudai mkataba wake baada ya Chippa kuuvunja kinyume cha sheria.
Banda alisema kukataa kupunguza mshahara ni sababu ya waajiri wake kusitisha mkataba na kuamua kukimbilia FIFA.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live