Tue, 31 Oct 2023
Chanzo: Voa
Balozi wa Uingereza nchini, David Concar anatarajia kutembelea mazoezi ya Simba SC leo katika Viwanja vya MO Simba Arena maeneo ya Bunju Jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Imani Kajula ameeleza kuwa, lengo la zaiara hiyo ni kuongeza nguvu katika soka la vijana lakini pia, amefurahi kuona Simba inavyoweka nguvu katika soka la wanawake.
"Amesema amevutiwa sana na mafanikio ya Simba na hii ni kutokana na mafanikio tuliyoyaonesha kwenye kombe la African Footbal League, tunakwenda naye Bunju aende akaione timu mazoezini," alisema Imani.
Chanzo: Voa