Tue, 13 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester City, Liverpool na Inter Milan ya Italia Mario Balotelli, amesema nyota wa kimataifa wa Ureno Cristiano Ronaldo anastahili heshima kwa aliyoyafanya kwenye mpira wa miguu bila kujali wewe ni shabiki yake au vinginevyo.
"Mimi sio shabiki wa Ronaldo na kila mtu analijua hilo ila kwa aliyoyafanya kwenye mpira anastahili kupewa heshima" amesema Balotelli
Kauli hiyo inakuja baada ya Ronaldo kushambuliwa kila kona na wapenda soka kutokana na matukio yake ya hivi karibuni ndani ya Man United na Timu ya Taifa ya Ureno.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live