Mshambuliaji wa zamani wa Vilabu vya AC Milan, Inter Milan, Man City na Liverpool Mario Baloteli Akizungumza Kwenye Podcast Ya Muschio Selvaggio, ameshangaza wengi baada ya kukiri kuwa ukosefu wake wa juhudi ulichangia Messi na Ronaldo kubeba Ballon D’or 12 Kwa Pamoja.
Katika mazungumzo yake Balloteli anasema;
“Raiola ( ambae ni ajenti wake wa zamani) aliniambia jambo hilo hilo.. Ikiwa Messi Na Cristiano Ronaldo wana Ballon D’or nyingi, ni kosa lako, una uwezo mkubwa na mpaka sasa unacheza na 20% tu ya uwezo wako"
"Alikuwa sahihi sana. maana mimi binafsi pia najiona nimecheza katika sehemu ndogo ya uwezo wangu"