Tue, 30 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Vijana wa Thomas Tuchel, Kikosi cha the Blues kimefanikiwa kunyakua tuzo ya timu bora ya mwaka.
Chelsea inabeba tuzo hiyo baada ya kushinda ubingwa wa Ulaya mbele ya vigogo kutoka England Manchester City.
Ni wazi kuwa Chelsea imestahili kupata tuzo hiyo kwa kuwa ni moja ya timu iliotoa wachezaji wengi ambao walikua wakiwania Tuzo ya Ballon D'or.
Wachezaji watano wa Chelsea waliingia katika kinyang'anyiro ambao ni Cesar Azpilicueta, Jorginho, Ngolo Kante, Mason Mount na Rumelu Lukaku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live