Thu, 7 Oct 2021
Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz
Baada ya kukaa nje ya uwanja muda mrefu kiungo wa Yanga, Mapinduzi Balama amesema pamoja na kuungana na wenzake ana kazi ngumu ya kufanya ili kupata namba ya kucheza.
Balama amekaa nje ya uwanja msimu mzima akisumbuliwa na enka aliyofanyiwa upasuaji mara mbili nchini Afrika Kusini.
Amesema ubora wa nyota walioongezewa nguvu kwenye nafasi anayocheza unampa wakati mgumu kuingia moja kwa moja kikosi cha kwanza akiwa bado anahitaji muda ili kuwa fiti zaidi
Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz