Wed, 29 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki kisiki wa Yanga SC, Ibrahim Bacca ameongezewa mkataba wake mpaka mwaka 2027.
Akizungumza na Wasafi FM, Afisa wa habari wa Yanga SC, Ally Kamwe, amesema uongozi umemuongezea mkataba huo kutokana na kutambua umuhimu wake kikosini.
"Bacca ni mchezaji mzuri, tumemuongezea mkataba mrefu zaidi kuwahi kutokea kwenye historia ya soka," alisema Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live