Beki kisi wa Yanga SC, Ibrahim Abdullah Bacca amewaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kule Mbarali kuwapa hamasa wapate matokeo mazuri kesho Jumatano, Oktoba 4, 2023 dhidi ya Ihefu FC.
Bacca amesema mchezo utakuwa mgumu lakini kama wachezaji wamejipanga kufanya vizuri ili kuendelea kufanya vizuri kwenye ligi kuu bila kutazama kuwa Ihefu ndiyo timu iliyoivunja unbeaten ya mechi 49 ya Yanga msimu uliopita.
"Wananchi wajitokeze kutoka maeneo yote, wenyeji wa Mbeya pia tunawakaribisha kutisapoti. Hii ni Ligi sio michuano ya CAF, sisi kila mechi morali iko juu, confidence ipo tangu tunasajiliwa.
"Sisi tushasahau ya Ihefu kuhusu msimu uliopita, huu ni msimu mpya, maandalizi ni mapya, wachezaji ni wapya ukichanganya na sisi wakongwe, mimi mkongwe ni miaka mitatu Yanga sasa hivi.