Mon, 29 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa kiungo wa Simba Sc, Babacar Sarr ametangazwa kama mchezaji mpya wa klabu ya JS Kabylie ya Algeria kama mchezaji huru baada ya kumalizana na Wekundu hao wa Msimbazi.
Babacar (27) raia wa Senegal anaungana na aliyekuwa kocha wa Simba Sc, Abdelhak Benchikha pamoja na aliyekuwa kiungo wa Simba Sc, Sadio Kanoute klabuni hapo.
NB: Si tuliambiwa Benchikha amesema wachezaji wa Simba Sc hawafundishiki? Sasa mbona anawakusanya huko Algeria?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live