Klabu ya Yanga imethibitisha kuwa Meneja wake wa Idara ya Habari na Mawasiliano Ally Kamwe alipata changamoto ya afya na kuwaishwa hospitali muda mfupi kabla ya mechi ya Yanga na CR Belouizdad kumalizika.
Klabu ya Yanga imethibitisha kuwa Meneja wake wa Idara ya Habari na Mawasiliano Ally Kamwe alipata changamoto ya afya na kuwaishwa hospitali muda mfupi kabla ya mechi ya Yanga na CR Belouizdad kumalizika. Imeelezwa kwamba Kamwe anaendelea vizuri kwa sasa baada ya kupatiwa matibabu na ameonesha kuimarika kiafya wakati alipotembelewa Hospitalini hapo na Rais wa Yanga Hersi Said, Makamu wa Rais wa Yanga Arafaj Haji, Wachezaji wa Yanga Pacome Zouzoua na Azizi Ki na Waziri wa Madini Anthony Mavunde.