Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Baada ya kulazimishwa sare, Man City yapata majanga tena

Pep 7 Baada ya kulazimishwa sare, Man City yapata majanga tena

Mon, 4 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola atakosa wachezaji wawili muhimu watakaposafiri kwenda Aston Villa kwenye Ligi ya Premia siku ya Jumatano.

Jack Grealish na Rodri walipata kadi zao za njano za tano katika mchezo wa jana walipolazimishwa sare ya 3-3 na Tottenham Jumapili.

Rodri, ambaye tayari ametumikia adhabu ya kutocheza mechi tatu msimu huu, alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Pedro Porro.

Grealish aliona njano kwa kupiga mpira mbali na hatakutana na klabu yake ya zamani. Hii inamaanisha kuwa watatumikia marufuku ya lazima ya mchezo mmoja katika Villa Park.

Kusimamishwa kwao kutakuwa pigo kwa kikosi cha Guardiola kutokana na kiwango cha Villa cha nyumbani kufikia sasa msimu huu.

Mabingwa hao wanakwenda kwenye mechi hiyo wakiwafuata Arsenal kwa alama tatu kileleni mwa jedwali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live