Wed, 22 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Azam FC. Iddi Selemani amefanyiwa Oparesheni ya Goti nchini Afrika ya Kusini kutokana na majeraha yaliyokuwa yakimkabili.
Kwa upasuaji huo, Nado atakosa sehemu yote iliyobaki ya msimu wa Ligi kuu Bara 2021/2022.
Nado aliumia katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar, Novemba 30 mchezo walioibuka na ushindi wa goli 1-0.
Kiungo huyo alipata majeraha ya kukatika mtulinga wa kati (Anterior Cruciate Ligament) wa goti lake la mguu wa kulia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live