Sun, 3 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Hayawi hayawi sasa yamekua. Baada ya sintofahamu kwa majuma kadhaa hatimaye Yanga wamekata mzizi wa fitina baada ya usiku huu kumtambulisha raia wa Ghana, Bernard Morisson kujiunga nao akitokea kwa mahasimu wao Simba SC.
Morisson aliekuwa Yanga hapo awali aliondoka na kujiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili , mkataba ambao unaisha Agosti 14 mwaka huu.
Tayari Yanga wameanza kuimarisha kikosi chao baada ya kumaliza msimu kwa mafanikio makubwa wakifanikiwa kubeba mataji matatu msimu wa 2021/2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live