Wananchi hawana shoo ndogo, unaambiwa safari hii Yanga SC wanakuja na paredi la ushindi kwa kutumia helkopta Mei 25, 2024.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amesema, paredi la mwaka huu limeongezewa ladha na Benki ya NBC baada ya kuongeza fedha katika shamrashamra za ubingwa.
"NBC wamesema mnataka nini ? Wananchi tukasema tunataka paredi la angani hivyo siku hiyo kombe letu litazungushwa angani Dar es Salaam nzima, kuanzia Kawe, Mbagala, Kariakoo na maeneo yote ya jiji kisha mchana kombe litatua pale uwanjani," alisema Kamwe.