Klabu ya Singida Big Stars FC rasmi imeuzwa kwa Japhet Mboto Makau Mkurugenzi wa Fountain Gate Sports Academy, ambaye kuanzia sasa atakuwa mmiliki mpya wa timu hiyo iliyomaliza nafasi ya nne kwenye ligi kuu ya NBC msimu wa 2022/23.
Klabu hiyo kwa sasa imebadilishwa Jina kutoka Singida Big Stars na itaitwa Singida Fountain Gate FC.
Tazama Video zinazoelezea uuzwaji wa Timu hiyo hapa chini;
FOUNTAIN GATE YAINUNUA SINGIDA BIG STARS
— Azam TV (@azamtvtz) June 14, 2023
Msikie John Kadutu ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Bodi ya Singida Fountain Gate FC akitaja sababu za kuuzwa kwa klabu hiyo ambayo inatarajiwa kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Singida Big Stars sasa itajulikana kama… pic.twitter.com/MI1texDSMv
"Tumechukua 100% ya umiliki wa Singida Big Stars" maneno ya Rais wa Singida Fountain Gate FC, Japhet Makau akieleza makubaliano yao katika manunuzi ya Timu ya Singida Big Stars.#AzamSportsUpdates #UnunuziwaKlabu #SingidaFountainGateFC pic.twitter.com/tThQK8LwlV
— Azam TV (@azamtvtz) June 14, 2023