Tue, 25 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wametangaza kumuongezea mkataba mpya kiungo wao mkabaji Mzamiru Yassin.
Kupitia ukurasa wao wa Instagram, Simba wamemtangaza mchana huu kwa kuwqeka picha yake na kusindikiza na ujumbe uliosomeka hivi.
"Mzamiru Yassin amesaini mkataba mpya kuendelea kusalia katika kikosi chetu."
Picha hiyo inaonesha Mzamiru ataendelea kuwepo Simba mpaka mwaka 2026 hivyo wamemuongezea mkataba wa miaka 2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live