Tue, 2 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Simba wameshusha straika mpya Mganda Steven Mukwala ambaye alikuwa akiichezea Asante Kotoko SC ya Ghana.
Mukwala amepewa mkataba wa mpaka mitatu hivyoi ataitumikia klabu hiyo mpaka mwaka 2027. Kwenye nafasi hiyo anayoicheza, wapo nyota wengine wa kigeni Pa Omari Jobe na Fredy Michael ambao hatma yao bado haijatangazwa.
Mukwala mwenye umri wa miaka 24, amewahi pia kuchezea Vipers SC kisha kutolewa kwa mkopo Maroons FC inayocheza Ligi Kuu ya Uganda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live