Mon, 1 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Matajiri wa Jiji, Klabu ya Azam FC, imethibitisha kuachana na mchezaji wake wa muda mrefu, Mudathir Yahya Abbas, baada ya mkataba wake kumalizika tangu Juni 30, mwaka huu.
Azam FC, imetumia mitandao yake ya kijamii kumtakia kila la heri mchezaji huyo katika kazi yake ya mpira na wamemkaribisha klabuni hapo wakati wowote.
Mudathir Yahaya alijiunga na Azam FC mwaka 2011, akidumu klabuni hapo kwa zaidi ya miaka 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live