Fri, 3 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa michezo nchini kupitia TV3, Alex Ngereza amedai kuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Stephanie Aziz Ki sio mzuri kwenye kupiga mipira ya kutenga kama ambavyo amekuwa akisifiwa na watu.
"Sio kwamba Azizi ki ni mzuri sana kwenye mipira ya kutenga 'hapana' ila magolikipa wetu wengi sio wazuri kuzuia mipira ya mbali.
"Hili sio tatizo la Tanzania ni tatizo la Magolikipa wengi kutoka Africa kwasababu hawakui kwenye misingi halisi ya soka," amesema Alex Ngereza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live