Baada ya janga la tetemeko la ardhi nchini Morocco lililosababisha mchezo kati ya timu ya taifa ya Liberia dhidi ya Burkinafaso kutochezwa ,kambi ya timu ya taifa ya Burkinafaso ipo salama na wametoka nchini Morroco na Kwasasa wapo Paris,ufaransa.
Akizungumza afisa habari wa Yanga Sc Ali Kamwe amesema, Aziz Ki yupo salama na wamewasiliana na shirikisho la soka la Burkinafaso kuona ni kwa namna gani Aziz Ki atarejea nchini Tanzania kujiunga na kambi kabla ya kwenda Rwanda kuwafuata Al Merreikh.
Kamwe amesema kuwa taarifa kuhusu nyota huyo zitatolewa ya kwamba ni lini atarejea na kujiunga na wenzake au atafikia nchini Rwanda moja kwa moja kwaajii ya mchezo huo dhidi ya Al Merreikh.