Kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Stephanie Aziz Ki ametoa hofu Mashabiki kuhusu Taarifa za yeye kuondoka kwenye MITAA ya Jangwani mwisho mwa msimu huu.
Aziz Ki amewatoa hofu Mashabiki wa Yanga wakati akijibu comment ya Moja ya shabiki aliekoment kwenye ukurasa wa instagram wa Azi ki akimuomba asiondoke
Shabiki huyo alietambulika kwa Jina la @fmkalati aliandika " Sasa naweza kulala ila usiondoke mpaka umetupa medali ya CAF Champions league".
Aziz Ki alimjibu shabiki huyo kwa kuandika;
"The president signed me here because he has the ambition with This clubs to win international trophies and you that I did not share I will not be here to do those why he believed in me and bring me back here to him first and for his committee who believed in me in good times and bad".
Kwa Tafsiri ya Kiswahili
“Rais wa Yanga alinisaini hapa kwa sababu ana nia na klabu hii ya kutwaa mataji ya kimataifa nikiwa na nyinyi kitu ambaocho sijafanya bado nisingweza kuwa hapa kama sio kufanya hayo ndio maana aliniamini na kunirudisha hapa yeye na kamati yake ambayo inaniaamini katika nyakati nzuri na mbaya".