Kiungo Mshambuliaji wa Yanga Stephane Aziz Ki ameshinda tuzo ya Mchezaji bora wa Ligi Kuu ya NBC (MVP) 2023/24 kwa kuwashinda Feisal Salum (Azam FC), Kipre Junior (Azam FC), Djigui Diarra (Yanga SC) na Lay Matampi (Coastal Union), Ibrahim Bacca (Yanga), Kouassi Yao (Yanga) na Mohamed Hussein (Simba SC).
Aziz Ki ametwaa tuzo tatu katika usiku wa tuzo za TFF (NBC PL)
1: Mfungaji bora
2: Kiungo bora
3: Mchezaji bora
Aziz Ki MVP 2023/2024 (NBC PL)
Blueberry travel ni miongoni mwa wadhamini waliotoa zawadi kwa (MVP)
Ukitoa pesa:
◉ Aziz Ki anatakiwa asafiri Kuelekea Dubai kula bata kwa siku nne.
◉ Gharama zote watalipa wao ikiwemo hoteli ya nyota (5), usafiri wa kifahari, chakula, nauli kwenda na kurudi.
◉ Pia anatakiwa kwenda na mpenzi wake, Hamisa Mobetto ameulizwa kama yuko tayari kwenda naye? Faster kajibu NDIYO.